BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER

BUNNER
Breaking News
recent

KUAPISHWA KWA BI ANNA ELISHA MGHWIRA

Rais wa  jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John  Pombe Magufuli amemuapisha aliyekuwa mgombea urais mwaka 2015 kupitia chama cha ACT wazalendo Bi Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro .

Bi Anna Elisha Mghwira amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Saidi Meck Sadiki aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo .

Akizungumza baada ya kumuapisha Rais Magufuli amemtaka Bibi Anna Elisha Mghwira kwenda kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kuondoa kero zinazowakabili wananchi wa Kilimanjaro bila kujali itikadi za vyama vyao vya siasa, dini, makabila na kanda wanazotoka.

"Mimi huwa siteui watu hivi hivi huwa naangalia uwezo wa mtu na wewe nimekuchunguza na nimejiridhisha kuwa una uwezo wa kuwatumikia wananchi nenda kachape kazi, kawaondolee kero wananchi wa Kilimanjaro, wapo watu watakaokusema na wengine watakuonea wivu “amesema Dkt Magufuli, baada ya kumuapisha katika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Bi Mghwira amemshukuru Rais kwa kumuamini na kumteua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na amemuahidi kuwa yupo tayari kwenda kufanya kazi ya kuwatumikia wananchi na kujenga Taifa.

"Ninasema hii ni heshima kwa Taifa letu ni heshima kwa umoja wa nchi yetu, ni heshima kwa siasa za umoja wa nchi yetu, kumekuwa na minong'ono mingi sana kuwa Rais analeta nini, kuteua watu wanaitwa wapinzani, mimi sio mpinzani wa maendeleo" amesema Bi Mghwira.

Bi Mghwira alikuwa mgombea pekee wa kike wakati wa kinyang'anyiro cha urais mwaka 2015 na amekuwa mwenyekiti wa chama cha ACT wazalendo chama ambacho ni kichanga Zaidi nchini Tanzania kilichoundwa mwaka 2014.


Mghwira mwenye umri wa miaka 56 anatoka mkoa wa Singida na  Baba yake alikuwa diwani na kiongozi chama cha Tanu ambacho kwa sasa kinajulikana kwa jina la  CCM.

No comments:

Powered by Blogger.